Ijumaa, 3 Agosti 2018

Mungu Anakamilisha Wale Wanaoufuata Moyo Wake



Mungu Anakamilisha Wale Wanaoufuata Moyo Wake
📚📚Mwenyezi Mungu alisema, "Kila kitu unachofanya, kila tendo, kila nia, na kila jibu lazima kiletwe mbele za Mungu. Hiyo ni, maisha yako ya kawaida ya kiroho, maombi yako, ukaribu wako na Mungu, kula na kunywa neno la Mungu, ushirika na ndugu na dada zako, kuishi maisha yako katika kanisa, na hata huduma yako katika ushirikiano wako ni vitu vyote ambavyo lazima viletwe mbele za Mungu na kuchunguzwa na Yeye. Ni matendo kama hayo ndiyo yatakayokusaidia kustawi katika maisha. Mchakato wa kukubali uchunguzi wa Mungu ni mchakato wa kutakaswa. Kadri unavyoukubali uchunguzi wa Mungu, ndivyo unavyotakaswa zaidi, kadri unavyokuwa katika uwiano na matakwa ya Mungu, ili kwamba hutasikia wito wa uasherati na ubhadhirifu, na moyo wako utaishi katika uwepo wa Mungu; kadri unavyokubali uchunguzi wa Mungu, ndivyo unavyomuaibisha Shetani na kuutelekeza mwili. Kwa hivyo, kukubali uchunguzi wa Mungu ni njia ambayo watu wanafaa kutenda. Haijalishi kile unachokifanya, hata katika ushirika na ndugu na dada zako, ukiyaleta matendo yako mbele za Mungu na kutafuta uchunguzi wa Mungu, na kama nia yako ni kumtii Mungu Mwenyewe, unachotenda ni sahihi zaidi. Kama tu wewe ni mtu anayeleta kila kitu anachofanya mbele za Mungu na kukubali uchunguzi wa Mungu ndipo utakapokuwa mtu anayeishi kwa hakika katika uwepo wa Mungu." kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni