Jumatano, 7 Februari 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II

Tabia ya Haki ya Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa vile sasa mumesikiliza kikao cha ushirika uliopita kuhusu mamlaka ya Mungu, Ninao ujasiri kwamba mumejihami vilivyo na mseto wa maneno kuhusu suala hili. Kiwango unachoweza kukubali, kushika, na kuelewa vyote hivi vinategemea na jitihada zipi utakazotumia. Ni tumaini Langu kwamba utaweza kutazamia suala hili kwa dhati; kwa vyovyote vile hufai kulishughulikia shingo-upande! Sasa, je, kujua mamlaka ya Mungu ni sawa na kujua Mungu kwa uzima wake?  Mtu anaweza kusema kwamba kujua mamlaka ya Mungu ndiyo mwanzo wa kumjua Mungu mwenyewe kwa upekee wake, na mtu anaweza kusema pia kwamba kuyajua mamlaka ya Mungu kunamaanisha kwamba mtu tayari ameingia kwenye lango kuu la kujua hali halisi ya ule upekee wa Mungu Mwenyewe. Ufahamu huu ni sehemu moja ya kumjua Mungu. Sehemu ile nyingine ni nini, hivyo basi? Hii ndiyo mada ambayo Ningependa tuweze kushiriki pamoja leo—tabia ya haki ya Mungu.
Nimeteua sehemu mbili kutoka kwenye Biblia ambazo ningependa tushiriki pamoja kuhusu mada ya leo: Jambo la kwanza linahusu kuangamizwa kwa Sodoma na Mungu, ambalo linaweza kupatikana kwenye Mwanzo 19:1-11 na Mwanzo 19:24-25; jambo la pili linahusu ukombozi wa Ninawi na Mungu, ambalo linaweza kupatikana kwenye kitabu cha Yona 1:1-2, kuongezea sura zile za tatu na nne za kitabu hiki. Ninashuku kwamba nyinyi nyote mnasubiri kusikia kile Nilicho nacho kuhusu sehemu hizi mbili. Kile Ninachosema hakiwezi kwenda kando na mada ya kutaka kumjua Mungu Mwenyewe na kujua hali Yake halisi, lakini ni nini kitakachokuwa zingatio la ushirika wa leo? Je, yupo yeyote kati yenu anayejua? Ni sehemu zipi za ushirika Wangu kuhusu “Mamlaka ya Mungu” ziliweza kuwavutia? Kwa nini Nilisema kwamba yule tu anayemiliki mamlaka na nguvu kama hizo ndiye Mungu mwenyewe? Ni nini Nilichotaka kuelezea kwa kusema hivyo? Ni nini ambacho Nilipenda kukufahamisha kuhusu? Je, mamlaka na nguvu za Mungu ni mtazamo mmoja unaoelezea kuhusu hadhi Yake halisi na inavyoonyeshwa? Je, mamlaka na nguvu hizi ni sehemu ya hali Yake halisi ambayo inathibitisha utambulisho Wake na hadhi? Je, maswali haya yamekufahamisha kile Ninachoenda kusema? Ni nini Ninachotaka uelewe? Fikiria hili kwa makini.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Biblia,

(I) Kwa Kupinga Mungu Kila Wakati, Binadamu Anaangamizwa na Hasira za Mungu

Kwanza, hebu tuweze kuangalia mafungu mbalimbali ya maandiko yanayofafanua “kuangamizwa kwa Sodoma na Mungu.”
(Mwa 19:1-11) Na wakaja malaika wawili Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma: na Lutu alipowaona akaondoka akaenda kuwalaki; akainama kifudifudi; Na akasema, tazama sasa, bwana zangu, ingieni ndani, nawasihi, ndani ya nyumba ya mtumwa wenu, na mlale usiku mzima, muoshe miguu yenu, na asubuhi muamke mwondoke na mapema mwende zenu. Wakasema, La; lakini tutakaa uwanjani usiku kucha. Na akawasihi sana; nao wakaja, na wakaingia katika nyumba yake; na akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyo na chachu, na wakala.
Lakini kabla hawajalala, watu wa mji, hata wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka sehemu zote: Na wakamwita Lutu, wakamwambia, Wako wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Walete kwetu, ili tuweze kuwajua. Lutu akaenda mlangoni walikokuwa, akafunga mlango nyuma yake. Na akasema, Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi. Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu wa kiume; niruhusu, nawasihi, nitawatolea kwenu muwafanyie vilivyo vizuri machoni penu: ila watu hawa msiwatende neno; kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha paa yangu. Wakasema, Ondoka. Kisha wakasema tena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni, naye kumbe anataka kuhukumu: basi tutakutenda wewe vibaya, kuliko vile tutawatenda hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, hata Lutu, hata wakakaribia kuuvunja mlango. Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu nyumbani walikokuwa, na wakaufunga mlango. Kisha wakawapiga hao watu waliokuwa mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa: kiasi kwamba wakachoka wasiweze kuutafuta mlango.
(Mwa 19:24-25) Kisha BWANA akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto kutoka mbinguni kwa BWANA; Na akaangusha miji hiyo, na bonde lote, na wakaaji wote wa miji hiyo, na yote yaliyomea kutoka katika nchi.
Kutoka kwenye mafungu haya, si vigumu kuona kwamba dhambi ya Sodoma na kupotoka kwake tayari vilikuwa vimefikia kiwango kilichochukiza binadamu na Mungu, na kwamba kwa macho ya Mungu mji ulifaa kuangamizwa. Lakini nini kilichofanyikia mji huu hapo awali kabla haujaangamizwa? Ni nini tunachoweza kujifunza kutoka kwenye matukio haya? Je, mtazamo wa Mungu katika matukio haya unatuonyesha nini kuhusu tabia yake? Ili kuelewa hadithi nzima, hebu na tuweze kusoma kwa makini kile kilichorekodiwa katika Maandiko ….

Kupotoka kwa Sodoma: Kunakasirisha Binadamu, Kunaghadhibisha Mungu

Kwenye usiku huo, Lutu alipokea wajumbe wawili kutoka kwa Mungu na akawatayarishia karamu. Baada ya chajio, kabla hawajalala, watu kutoka kila pahali kwenye mji walizunguka makazi ya Lutu na kumwita nje Lutu. Maandiko yanawarekodi wakisema, “Wako wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Walete kwetu, ili tuweze kuwajua..” Ni nani aliyesema maneno haya? Alikuwa akiwaambia kina nani? Haya yalikuwa maneno ya watu wa Sodoma, walipiga mayowe nje ya makazi ya Lutu wakinuia kumwita Lutu. Je, unahisi vipi ukiyasikia maneno haya? Unaghadhibishwa? Je, maneno haya yanakuhuzunisha? Je, unabubujikwa na hasira kali? Je, Huoni kwamba maneno haya yananuka Shetani? Kupitia kwa maneno haya, unaweza kuhisi uovu na giza vilivyomo kwenye mji huu? Je, unaweza kuhisi ukatili na ushamba wa tabia za watu hawa kupitia kwa maneno yao? Je, unaweza kuhisi kina cha kupotoka kwao kupitia kwa tabia yao? Kupitia kwa maudhui ya hotuba yao, si vigumu kuona kwamba asili yao ya dhambi na tabia yao iliyopotoka ilikuwa imefikia kiwango kilichokuwa zaidi ya wao kuidhibiti. Isipokuwa Lutu, kila mtu katika mji huu hakuwa tofauti na Shetani; ule mtazamo tu wa mtu mwengine uliwafanya watu hawa kutaka kudhuru na kuwapotosha wao…. Mambo haya hayampatii tu mtu hisia ya asili potoshi na ya kutisha ya mji huu, lakini pia yanamwonyesha harufu ya kifo iliyouzunguka mji huu; yanampa pia mtu hisia za dhambi na umwagikaji wa damu.
Alipojipata uso-kwa-uso na genge la majambazi waliojaa ukatili, watu waliokuwa wamejaa na maono ya kupotosha-nafsi, Lutu aliitikia vipi? Kulingana na Maandiko: “Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi. Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu wa kiume; niruhusu, nawasihi, nitawatolea kwenu muwafanyie vilivyo vizuri machoni penu: ila watu hawa msiwatende neno; kwa kuwa wamekuja chini ya kivuli cha paa yangu.” Lutu alimaanisha yafuatayo katika maneno yake: Alikuwa radhi kuwatoa binti zake wawili ili kuwalinda wale wajumbe. Kutokana na akili razini, watu hawa wangekubali masharti ya Lutu na kuwaacha wale wajumbe wawili pekee; kwani hata hivyo, wajumbe hao walikuwa watu wageni kabisa kwao, watu ambao hawakuwa na chochote katu kuhusiana na wao; wajumbe hawa wawili walikuwa hawajawahi kudhuru masilahi yao. Hata hivyo, wakiwa na motisha ya asili yao ya dhambi, hawakuliwachia suala hili hapo. Badala yake, walizidisha tu jitihada zao. Hapa mojawapo ya mabishano yao yanaweza bila shaka kumpatia mtu maono zaidi kuhusu asili ya kweli na potoshi ya watu hawa; wakati uo huo yanatujuza na kutufanya tuelewe sababu ya Mungu kutaka kuuangamiza mji huu.
Kwa hivyo walisema nini baadaye? Kama vile Biblia inavyosoma: “Ondoka. Kisha wakasema tena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni, naye kumbe anataka kuhukumu: basi tutakutenda wewe vibaya, kuliko vile tutawatenda hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, hata Lutu, hata wakakaribia kuuvunja mlango.” Kwa nini walitaka kuuvunja mlango? Sababu ni kwamba walikuwa na hamu kubwa zaidi ya kuwadhuru wale wajumbe wawili. Wale wajumbe walikuwa wakifanya nini Sodoma? Kusudio lao la kuja hapo lilikuwa ni kumwokoa Lutu na familia yake; hata hivyo, watu wa mji huo walifikiri kimakosa kwamba walikuwa wamekuja kuchukua nyadhifa zao rasmi. Bila ya kuulizia kusudio lao, ilikuwa tu hali ya kujiamulia kufanya mambo kabla ya kujua ukweli wake, iliyoufanya mji huo kutaka kuwadhuru vibaya wajumbe hawa wawili; walitaka kuwadhuru watu wawili ambao hawakuhusiana kwa vyovyote vile na wao. Ni wazi kwamba watu wa mji huu walikuwa wamepoteza kabisa ubinadamu na akili zao razini. Kiwango cha wendawazimu wao na kukosa ustaarabu kwao kilikuwa tayari si tofauti na asili potoshi ya Shetani ya kudhuru na kudanganya binadamu.
Walipowaamuru watu hawa watoke kwa Lutu, Lutu alifanya nini? Kutoka kwenye maandishi yanayofuata tunajua kwamba Lutu hakuwakabidhi wajumbe hawa kwa watu hawa. Je, Lutu aliwajua wajumbe hawa wawili wa Mungu? Bila shaka la! Lakini kwa nini aliweza kuwaokoa watu hawa wawili? Je, alijua ni nini walichokuwa wamekuja kufanya? Ingawaje hakujua kuhusu sababu yao ya kuja, alijua kwamba walikuwa ni watumishi wa Mungu, na kwa hivyo aliwapokea. Kwamba aliweza kuwaita watumishi hawa wa Mungu mabwana yaonyesha kwamba Lutu kwa kawaida alikuwa ni mfuasi wa Mungu, tofauti na wale wengine waliokuwa ndani ya Sodoma. Kwa hivyo, wakati wajumbe wa Mungu walipomjia, alihatarisha maisha yake binafsi ili kuwapokea watumishi hao wawili; aidha, aliwakabidhi binti zake wawili badala ya watumishi hao wawili ili kuwalinda watumishi hao. Hiki ndicho kitendo cha haki ya Lutu; vilevile ni onyesho linaloonekana waziwazi kuhusu asili na hali halisi ya Lutu, na ndiyo pia sababu ya Mungu kuwatuma watumishi Wake ili kumwokoa Lutu. Wakati alipokabiliwa na changamoto, Lutu aliwalinda watumishi hawa wawili bila kujali chochote kingine; alijaribu hata kufanya biashara ya kuwabadilisha binti zake wawili mradi tu watumishi hawa wapate usalama. Mbali na Lutu, kulikuwa na mtu yeyote mwengine ndani ya mji ambaye angefanya jambo kama hili? Kama vile hoja zinavyothibitsha—la! Kwa hivyo, ni wazi kabisa kwamba kila mtu katika Sodoma, isipokuwa Lutu, alikuwa mlengwa wa kuangamizwa pamoja na mlengwa aliyestahili kuangamizwa.

Sodoma Yaangamizwa kwa Kuchochea Hasira za Mungu

Wakati watu wa Sodoma walipowaona watu hawa wawili, hawakuuliza sababu ya wao kuja wala hakuna yule aliyeuliza kama walikuwa wamekuja kueneza mapenzi ya Mungu. Kinyume cha mambo, walikusanyika na kuwa umati wa watu na, bila kusubiri ufafanuzi wowote, walikuja kuwakamata watumishi hawa wawili ni kana kwamba walikuwa mbwakoko au mbwa mwitu. Je, Mungu aliyatazama mambo haya wakati yalipokuwa yakifanyika? Mungu alikuwa akifikiria nini katika moyo Wake kuhusiana na tabia hii ya binadamu, aina ya jambo hili? Mungu aliamua kuangamiza mji huu; Asingesita wala kusubiri, wala Asingeendelea kuonyesha subira yake. Siku yake ilikuwa imetimia, na kwa hivyo Aliweza kuweka wazi kazi Aliyopenda kufanya. Hivyo basi, Mwanzo 19:24-25 inasema, “Kisha BWANA akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto kutoka mbinguni kwa BWANA; Na akaangusha miji hiyo, na bonde lote, na wakaaji wote wa miji hiyo, na yote yaliyomea kutoka katika nchi.” Mistari hii miwili inawaambia watu mbinu ambayo kwayo Mungu aliuangamiza mji huu; pia inawaambia watu kile ambacho Mungu aliangamiza. Kwanza, Biblia inasimulia kwamba Mungu aliunguza mji kwa moto, na kwamba kiwango cha moto kilikuwa tosha kuangamiza watu wote na kila kitu kilichomea kwenye ardhi. Hii ni kusema kwamba, moto ulioangushwa kutoka mbinguni haukuangamiza tu mji; uliangamiza pia watu wote na vitu vilivyo hai ndani yake, vyote bila kuacha chochote nyuma. Baada ya mji kuangamizwa, ardhi ilikuwa tupu bila kitu chochote kilicho hai. Hakukuwa tena na maisha, wala dalili zozote za maisha. Mji ulikuwa umebadilika na kuwa ardhi iliyoharibiwa, mahali patupu palipojaa kimya cha kutisha. Kusingekuwa na matendo maovu zaidi dhidi ya Mungu mahali hapa; kusingekuwa na uchinjaji zaidi au umwagikaji wa damu.
Kwa nini Mungu alitaka kuuchoma mji huu kabisa? Ni nini unachoweza kuona hapa? Je, Mungu angevumilia kumwona mwanadamu na asili, viumbe Vyake mwenyewe, vikiangamia hivi? Kama unaweza kutambua ghadhabu ya Yehova Mungu kutokana na moto ule ambao uliangushwa kutoka mbinguni, basi si vigumu sana kuona kiwango Chake cha hasira kali kutoka kwenye lengo la maangamizo Yake pamoja na kiwango ambacho mji huo uliweza kuangamizwa. Wakati Mungu anadharau mji, Ataweza kutekeleza adhabu Yake juu ya mji huo. Wakati Mungu anachukizwa na mji, Ataweza kutoa maonyo mbalimbali akifahamisha watu kuhusu ghadhabu Yake. Hata hivyo, wakati Mungu anaamua kukomesha na kuangamiza mji—yaani, wakati hasira Yake na adhama vimekosewa—Hataweza kutoa maonyo au adhabu nyingine. Badala yake, Ataweza kuuangamiza moja kwa moja. Ataufanya kutoweka kabisa. Hii ndiyo tabia ya haki ya Mungu.
kutoka kwa Mwendelezo wa Neno Laonekana katika Mwili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni