Jumamosi, 8 Desemba 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Swahili Christian Video "Kuzinduka" | Ni nini Maana ya Uzima?

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Swahili Christian Video "Kuzinduka" | Ni nini Maana ya Uzima?

Jina lake ni Chen Xi, na tangu akiwa mtoto elimu na ushawishi wa wazazi wake na shule yake zilimfanya yeye mara zote kutaka kwa tofauti na wengine na kutafuta kuwa juu ya wengine,kwa hivyo alikuwa na bidii katika masomo yake na kutia juhudi zote. Baada ya kumwamini Mungu Chen Xi alisoma maneno ya Mungu kwa wingi na akaja kuelewa kiasi fulani cha ukweli. Aliona kuwa njia pekee inayofaa katika maisha ni kumwamini na kumfuata Mungu na kuwa mtafutaji mwenye shauku, na alijitolea kwa dhati katika kutekeleza wajibu wake. Chen Xi alienda ughaibuni mwaka 2016 ili kutoroka harakati na mateso ya serikali ya Kikomunisti ya Kichina, na alihitaji kutumia Kiingereza wakati akifanya kazi yake ya kueneza injili na kutoa ushuhuda kwa kazi ya Mungu katika zile siku za mwisho. Alihisi kuheshimiwa, na kwamba alikuwa na talanta nadra. Kama vile alivyojazwa na kujiamini na alikuwa anafikiria kujitengenezea nafasi kanisani, aligundua kwamba ndugu na dada zake walishiriki ushirika kwa maneno ya Mungu kwa nuru na kwamba walikuwa na ufahamu zaidi wa Kiingereza kumliko. Yeye hakutaka kubaki nyuma, kwa hivyo ili kuwapita wengine na kutambuliwa na kupongezwa nao, alirudufu tena jitihada zake za kujifunza. Kipindi kidogo kilipita lakini bado hakuwafikia wengine. Chen Xi hakukubali ukweli huu na alijikuta akiishi kila siku kwa maumivu ya kujitahidi kwa ajili ya jina lake na faida yake binafsi. Yeye hakuwa na moyo wa kufuata ukweli au kuzingatia kuingia katika uzima, na alikuwa hasa hawezi kutekeleza wajibu wake vizuri. Alianguka kwa maono mabaya na kuvunjika moyo.... Ni wakati huo ndipo alikuja mbele za Mungu kwa sala na kusoma maneno Yake - hukumu na adhabu ya maneno Yake iliamsha nafsi yake na kumruhusu kuona wazi kiini cha sifa na hadhi pamoja na matokeo ya kufungwa na kuteswa na mambo haya. Alikuja kuelewa umuhimu wa kutekeleza wajibu wake, thamani ya kweli ya maisha, na maisha ya aina gani ndiyo ya furaha ya kweli. Kuanzia wakati huo alianza kuwa na malengo sahihi ya kufuata na kutokuwa chini ya fikira za uso au hadhi. Pia alianza kuzingatia kufuata ukweli na kutimiza wajibu wa kiumbe wa kulipa upendo wa Mungu
Maneno Husika ya Mungu:
"Hivyo ni nini malengo husuda ya Shetani? Hujayaelewa, sio? Katika mchakato wa mwanadamu kujifunza maarifa, Shetani atatumia mbinu zozote ili watu waridhishe tamaa yao wenyewe na kutambua maadili yao. Je, uko wazi kuhusu njia hasa anayotaka Shetani kukuongoza? Bila kutia chumvi, watu wanafikiri kwamba hakuna chochote kibaya na kujifunza maarifa, kwamba ni mkondo wa kiasili. Wanafikiri kwamba kukuzaa maadili ya juu ama kuwa na matarajio kunaitwa tu kuwa na hamu ya kupata, na kwamba hii inapaswa kuwa njia sawa ya watu kufuata katika maisha. Iwapo watu wanaweza kupata maadili yao wenyewe, ama kuwa na kazi maishani—je, si ni adhimu zaidi kuishi namna hii? Sio tu kuheshimu babu za mtu kwa njia hiyo bali pia kuacha alama yako katika historia—hili si jambo zuri? Hili ni jambo zuri na linalofaa katika macho ya watu wa kidunia. Je, Shetani, hata hivyo, na malengo yake husuda, anawapeleka watu kwa njia ya aina hii na kisha kuamua amemaliza? Bila shaka la. Kwa kweli, haijalishi jinsi yalivyo juu maadili ya mwanadamu, haijalishi matamanio ya mwanadamu ni ya uhalisi jinsi gani ama jinsi yote yanaweza kuwa ya kufaa, yote ambayo mwanadamu anataka kufikia, yote ambayo mwanadamu anatafuta yameunganishwa bila kuchangulika na maneno mawili. Haya maneno mawili ni muhimu sana kwa maisha ya kila mtu, na haya ni mambo ambayo Shetani ananuia kuingiza ndani ya mwanadamu. Maneno haya mawili ni yapi? Moja ni “umaarufu” na nyingine ni “faida”: Ni umaarufu na faida. Shetani anatumia njia ya hila sana, njia ambayo iko pamoja sana na dhana za watu; si aina ya njia kali. Katikati ya kutoelewa, watu wanakuja kukubali njia ya Shetani ya kuishi, kanuni zake za kuishi, kuanzisha malengo ya maisha na mwelekeo wao katika maisha, na kwa kufanya hivyo wanakuja pia bila kujua kuwa na maadili katika maisha. Haijalishi maadili haya yanaonekana kusikika kuwa ya juu kiasi gani katika maisha, ni kisingizio tu ambacho kinahusiana kwa kutochangulika kwa umaarufu na faida. Mtu yeyote aliye mkubwa ama maarufu, watu wote kwa hakika, chochote wanachofuata maishani kinahusiana tu na haya maneno mawili: “umaarufu” na “faida.” Sivyo? (Ndiyo.) Watu hufikiri kwamba punde tu wanapata umaarufu na faida, wanaweza basi kuyatumia kwa faida yao kufurahia hadhi ya juu na utajiri mwingi, na kufurahia maisha. Baada ya wao kuwa na umaarufu na faida, wanaweza basi kuyatumia kwa faida yao katika kutafuta kwao raha na kufurahia kwao kwa fidhuli mwili. Watu kwa hiari, lakini bila kujua, wanachukua miili na akili zao na vyote walivyonavyo, siku zao za baadaye, na kudura zao na kuzikabidhi zote kwa Shetani ili kupata umaarufu na faida wanayotaka. Watu hufanya hivi kamwe bila kusita kwa muda, kamwe bila kujua haja ya kupata tena yote. Je, watu bado wanaweza kujidhibiti baada ya wao kwenda upande wa Shetani kwa njia hii na kuwa mwaminifu kwake? Bila shaka, la. Wanadhibitiwa na Shetani kikamilifu na kabisa. Hawawezi kikamilifu na kabisa kujinusuru kutoka kwa bwawa ambamo wamezama ndani. Baada ya mtu kukwama katika umaarufu na faida, hatafuti tena kile kilichong’aa, kile chenye haki ama yale mambo ambayo ni mazuri na mema. Hii ni kwa sababu nguvu za ushawishi ambazo umaarufu na faida yanayo juu ya watu ni kubwa mno, na vinakuwa vitu vya watu kutafuta katika maisha yao yote na pia milele bila kikomo. Hili silo ukweli?"
kutoka katika Mwendelezo wa Neno Laonekana katika Mwili
Tazama Video: Filamu za Injili
Tufuate: Kuhusu Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni