Jumanne, 4 Desemba 2018

Sura ya 6 Aina Mbalimbali za Utofautishaji Ambazo Unafaa Kumiliki katika Kusadiki Kwako kwa Mungu | Unafaa Utofautishe Vipi Kati ya Kazi ya Roho Mtakatifu na Kazi ya Pepo Wabaya?

2. Unafaa Utofautishe Vipi Kati ya Kazi ya Roho Mtakatifu na Kazi ya Pepo Wabaya?

Maneno Husika ya Mungu:
Mwenyezi Mungu alisema, Kazi ya Roho Mtakatifu ni kuhusu kuwasaidia watu kupata faida; ni kuwaadilisha watu; hakuna kazi ambayo haiwanufaishi watu. Haijalishi kama ukweli ni wa kina au usio wa kina, na haijalishi tabia ya wale wanaopokea ukweli huo ilivyo, chochote ambacho Roho Mtakatifu Anafanya, yote hayo huwanufaisha watu.
kutoka kwa "Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Kazi ya Roho Mtakatifu ni aina ya mwongozo wa kimatendo na kupata nuru kwa hali nzuri. Haiwaruhusu watu kuwa baridi. Huwaletea faraja, huwapa imani na uamuzi na kuwawezesha kufuatilia kufanywa kamili na Mungu. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi, watu wanaweza kuingia kwa vitendo; wao si baridi wala hawalazimishwi, lakini ni wa kimatendo. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi, watu wana faraja na wenye radhi, na wako tayari kutii, na wana furaha kujinyenyekeza, na hata ingawa wana maumivu na ni dhaifu ndani, wana uamuzi wa kushirikiana, wanateseka kwa furaha, wanaweza kutii, na hawajatiwa doa na mapenzi ya mwanadamu, hawajatiwa doa na fikira ya mwanadamu, na hakika hawajatiwa doa na tamaa na motisha za mwanadamu. Wakati watu wanapitia kazi ya Roho Mtakatifu, ndani yao ni watakatifu hasa. Wale ambao wanamiliki kazi ya Roho Mtakatifu huishi kwa kudhihirisha upendo wa Mungu, upendo wa kaka na dada zao, na kufurahia vitu ambavyo Mungu hufurahia na kuchukia vitu ambavyo Mungu huchukia. Watu ambao wanaguswa na kazi ya Roho Mtakatifu wana ubinadamu wa kawaida, na wanamiliki ubinadamu na daima hufuatilia ukweli. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi ndani ya watu, hali zao huwa nzuri zaidi na zaidi, na ubinadamu wao unakuwa wa kawaida zaidi na zaidi, na ingawa ushirikiano wao mwingine unaweza kuwa mpumbavu, motisha zao ziko sahihi, kuingia kwao ni kwa hali nzuri, hawajaribu kukatiza, na hakuna nia mbaya ndani yao. Kazi ya Roho Mtakatifu ni ya kawaida na ya kweli, Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa mwanadamu kulingana na amri za maisha ya kawaida ya mwanadamu, na Yeye huwapa nuru na kuongoza watu kulingana na ufuatiliaji halisi wa watu wa kawaida. Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa watu, Yeye huwaongoza na kuwapa nuru kulingana na mahitaji ya watu wa kawaida, Anawakimu kwa msingi wa mahitaji yao, na Yeye huwaongoza na kuwapa nuru kwa hali nzuri kwa msingi wa kile ambacho wanakosa, na kwa upungufu wao; wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi, kazi hii inalingana na amri za maisha ya kawaida ya mwanadamu, na ni katika maisha halisi pekee ndio watu wanaweza kuona kazi ya Roho Mtakatifu. Iwapo, katika maisha yao ya kila siku, watu wako katika hali nzuri na wana maisha ya kawaida ya kiroho, basi wanamiliki kazi ya Roho Mtakatifu. Katika hali kama hiyo, wakati wanakula na kunywa maneno ya Mungu wana imani, wakati wanaomba wanatiwa moyo, wakati kitu kinawafanyikia wao si baridi, na wakati kinawafanyikia wanaweza kuona masomo ambayo Mungu anawahitaji kujifunza, na hawako baridi, ama dhaifu, na ingawa wana ugumu wa kweli, wako tayari kukubali mipango yote ya Mungu.
…………
Ni kazi ipi hutoka kwa Shetani? Katika kazi inayotoka kwa Shetani, maono ndani ya watu si yakini na ni dhahania, na hawana ubinadamu wa kawaida, motisha za vitendo vyao si sahihi, na ingawa wanataka kumpenda Mungu, daima kuna lawama ndani yao, na lawama hizi na fikira daima zinaingilia katindani yao, zikizuia kukua kwa maisha yao, na kuwasitisha kuwa na hali za kawaida mbele ya Mungu. Ambayo ni kusema, punde tu kuna kazi ya Shetani ndani ya watu, mioyo yao haiwezi kuwa kwa amani mbele ya Mungu, na hawajui cha kufanya, kuona mkutano kunawafanya kutaka kuhepa, na hawawezi kufumba macho yao wakati wengine wanaomba. Kazi ya roho waovu huharibu uhusiano wa kawaida kati ya mwanadamu na Mungu, na huvuruga maono ya awali ya watu na njia ambayo maisha yao yameingia, katika mioyo yao hawawezi kamwe kumkaribia Mungu, daima mambo hufanyika ambayo huwasababishia vurugu na kuwatia pingu, na mioyo yao haiwezi kupata amani, kuacha upendo wao wa Mungu bila nguvu, na kuwafanya kusononeka. Hayo ndiyo maonyesho ya kazi ya Shetani. Kazi ya Shetani inadhihirishwa katika yafuatayo: kutoweza kushikilia msimamo na kuwa na ushuhuda, kukusababisha kuwa mtu ambaye ana makosa mbele ya Mungu, na ambaye hana uaminifu kwa Mungu. Kwa kuingilia kwa Shetani, unapoteza upendo na uaminifu kwa Mungu ndani yako, unaondolewa uhusiano wa kawaida na Mungu, hufuatilii ukweli, ama kujiendeleza, unarudi nyuma, na kuwa baridi, unajipendeza, unaachia uenezaji wa dhambi, na huchukii dhambi; zaidi ya hayo, kuingilia kwa Shetani kunakufanya mpotovu, kunasababisha mguso wa Mungu kutoweka ndani yako, na kunakufanya kulalamika kuhusu Mungu na kumpinga Yeye, kukufanya uwe na shaka na Mungu, na hata kuna hatari ya wewe kumwacha Mungu. Hii yote ni kazi ya Shetani.
kutoka kwa "Kazi ya Roho Mtakatifu na Kazi ya Shetani" katika Neno Laonekana katika Mwili
Ikiwa ni kazi ya Roho Mtakatifu, mwanadamu anakuwa wa kawaida kabisa, na ubinadamu wake unakuwa wa kawaida kabisa. Mwanadamu ana maarifa mengi ya tabia yake, ambayo yameharibiwa na Shetani, na asili ya mwanadamu, na ana shauku kubwa ya kuuelewa ukweli. Ni sawa na, kusema, maisha ya mwanadamu yanakuwa na kukua, na Atabia ya upotovu ya mwanadamu inakuwa na uwezo wa mabadiliko zaidi na zaidi—yote hiyo ni maana ya Mungu kuwa maishi ya mwanadamu. Kama njia haiwezi kufunua vitu hivyo ambavyo ni asili ya mwanadamu, haiwezi kubadilisha atabia ya mwanadamu, na, zaidi ya hayo, hauwezi kumleta mbele ya Mungu au kumpa uelewa wa kweli juu ya Mungu, na hata kufanya ubinadamu wake kuwa duni zaidi na hisia zake kuwa si za kawaida zaidi, basi njia hii itakuwa si njia ya kweli, na inaweza kuwa ni kazi ya roho mchafu, au njia ya zamani. Kwa ufupi, haiwezi kuwa kazi ya sasa ya Roho Mtakatifu.
kutoka kwa "Ni Wale tu Wanaomjua Mungu na Kazi Yake ndio Wanaoweza Kumridhisha Mungu" katika Neno Laonekana katika Mwili
Mambo yanayotokana na Mungu hukusababisha kuwa wazi zaidi kuhusu maono, na hukusababisha kusogea karibu na karibu zaidi na Mungu, ukishiriki upendo na ndugu kwa bidii; unakuwa na uwezo wa kutilia maanani mzigo wa Mungu, na moyo wako umpendao Mungu haupungui; kuna njia mbele yako kuitembea. Mambo ambayo hutokana na Shetani hukusababisha kupoteza maono na vyote ulivyokuwa navyo awali vimetoweka; unajitenga na Mungu, huna upendo kwa ndugu nawe una moyo wa chuki. Unakuwa mwenye kukata tamaa, hutaki tena kuishi maisha ya kanisa, na moyo wako umpendao Mungu hauko tena. Hii ni kazi ya Shetani na pia ni matokeo ambayo yameletwa na kazi ya roho mbaya.
kutoka kwa Matamshi na Ushuhuda wa Kristo Mwanzoni
Wakati Roho Mtakatifu hufanya kazi ili kuwapa watu nuru, Yeye kwa ujumla kuwapa ufahamu wa kazi ya Mungu, na ya kuingia kwao ya kweli na hali ya ukweli, na pia Huwapa azimio, huwaruhusu kuelewa kusudi la hamu la Mungu na mahitaji yake kwa ajili ya mtu leo, Huwapa azimio la kufungua njia zote. Hata wakati ambapo watu wanapitia umwagaji damu na sadaka ni lazima watende kwa ajili ya Mungu, na hata kama wanakumbana na mateso na dhiki, lazima bado wampende Mungu, na wasiwe na majuto, na lazima wawe shahidi kwa Mungu. Azimio la aina hii ni misisimko ya Roho Mtakatifu, na kazi ya Roho Mtakatifu—lakini jua kwamba hujamilikiwa na misismko kama hii kila wakati.
kutoka kwa "Utendaji (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Watu wengine husema kwamba Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yao nyakati zote. Hili haliwezekani. Ikiwa wangesema kwamba Roho Mtakatifu yuko nao kila mara, hilo lingekuwa la kweli. Ikiwa wangesema kwamba fikira na hisi zao ni za kawaida nyakati zote, hilo pia lingekuwa la kweli, na lingeonyesha kwamba Roho Mtakatifu yuko nao. Ikiwa unasema kwamba Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yako kila mara, kwamba unapata nuru kutoka kwa Mungu na kuguswa na Roho Mtakatifu kila wakati, na unapata ufahamu mpya kila wakati, basi hili si la kawaida. Ni la rohoni kabisa! Bila tashwishi yoyote, watu hao ni pepo wabaya! Hata wakati ambapo Roho wa Mungu huja ndani ya mwili, kuna nyakati ambapo lazima Apumzike, na lazima Ale—sembuse wewe. Wale ambao wamemilikiwa na pepo wabaya huonekana kutokuwa na udhaifu wa mwili. Wanaweza kutelekeza na kuacha kila kitu, wao ni wasiohemkwa, wenye uwezo wa kustahimili mateso, wao hawahisi uchovu hata kidogo sana, kana kwamba wamevuka mipaka ya mwili. Je, hili silo la rohoni kabisa? Kazi ya pepo mwovu ni ya rohoni, na mambo haya ni yasiyofikiwa na mwanadamu. Wale wasioweza kutofautisha huwa na wivu wanapoona watu kama hao, na husema kwamba imani yao katika Mungu ni thabiti sana, na nzuri sana, na kwamba wao huwa si wadhaifu kamwe. Kwa kweli, hili ni dhihirisho la kazi ya pepo mwovu. Hiyo ni kwa sababu watu wenye hali ya kawaida huwa na udhaifu wa binadamu usioepukika; hii ni hali ya kawaida ya wale walio na kuwepo kwa Roho Mtakatifu.
kutoka kwa "Utendaji (4)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Wanaweza kuzungumza kutoka ndani mwako au ndani ya sikio lako, au la sivyo wanaweza kuyachanganya mawazo na akili yako, wanazuia kuguswa kwa Roho Mtakatifu ili usiweze kuuhisi, na baada ya hapo wanaanza kukuingilia, kuzifanya fikira zako ziwe zilizochanganyikiwa na akilia yako iwe iliyovurugika, na kukufanya usiyekuwa na utulivu na usiye thabiti. Hivyo ndivyo ilivyo kazi ya roho wabaya.
kutoka kwa "Maana ya Mungu Kuupitia Uchungu wa Dunia" katika Neno Laonekana katika Mwili
Unaweza kuhisi roho yako mwenyewe? Unaweza kugusa roho yako? Unaweza kuhisi roho yako inafanya nini? Hujui, siyo? Ikiwa unaweza kuhisi na kugusa  vitu fulani kama hiki, basi ni roho nyingine ndani yako inafanya kitu kwa nguvu—ikidhibiti vitendo na maneno yako. Ni kitu kisichohusiana na wewe, kisicho cha wewe. Wale wenye roho ovu wana uzoefu wa kina na hili.
kutoka kwa "Jinsi ya kuelewa Umoja wa Mwili wa Mungu na Roho" katika Neno Laonekana katika Mwili
Leo kunao baadhi ya pepo wabaya wanaofanya kazi kupitia kwa mambo yasiyo ya ulimwenguni humu ili kumpotosha mwanadamu; hilo si chochote bali ni uigaji kwa upande wao, kumpotosha mwanadamu kupitia kwa kazi ambayo kwa sasa haifanywi na Roho Mtakatifu. Pepo wengi wabaya huiga ufanyaji wa miujiza na uponyaji wa magonjwa; si chochote ila kazi ya pepo wabaya, kwani Roho Mtakatifu hafanyi tena kazi kama hiyo leo. Wale wote wanaokuja baadaye na wanaoiga kazi ya Roho Mtakatifu—ni pepo wabaya.
kutoka kwa "Fumbo la Kupata Mwili (1)" katika Neno Laonekana katika Mwili
Ushirika wa Mtu:
Kazi ya Roho Mtakatifu huwaruhusu watu kuuelewa ukweli, huwaruhusu kujua kiini potovu cha Shetani, na huwapa maarifa ya kweli kuhusu kile Mungu anacho na Alicho. Athari zake zote ni nzuri kwa ujumla. Leo, tunajua ukweli ni nini, kwamba ukweli unatoka kwa Mungu, kwamba mambo mazuri yanatoka kwa Mungu, kile kinachofaa kumilikiwa na watu wenye ubinadamu wa kawaida, kile ambacho ni mapenzi ya Mungu, na kile ambacho ni maisha ya kweli. Mambo haya yote ni mazuri, na uhalisi wa mambo mazuri ni ukweli. Hivi ndivyo athari ya kazi ya Mungu ilivyo, na tunaielewa tu kutokana na kupata nuru na uangazaji wa Roho Mtakatifu. Kazi ya pepo wabaya haiwezi kuwapa watu maarifa ya mambo mazuri. Unafaa kuwa wazi na kujua kwamba watu ambao pepo wabaya hufanya kazi ndani yao hawaelewi wala kuufahamu ukweli wowote. Kazi ya pepo wabaya inaweza tu kuwafanya watu kuwa waovu zaidi na zaidi, inaweza kuleta tu giza zaidi na zaidi ndani ya mioyo yao, kuzifanya tabia zao kuwa potovu zaidi na zaidi, na hali yao kuzoroteka zaidi na zaidi, na hatimaye kuishia katika kuteseka milele na kuangamia. Kazi ya Roho Mtakatifu huwafanya watu kuwa wa kawaida zaidi na zaidi, huwapa ufahamu mkubwa zaidi wa ukweli na siku zote huwapa imani kubwa zaidi kwa Mungu, na wanaweza kumtii Mungu zaidi na zaidi. Hatimaye, huwaruhusu kumjua kabisa Mungu na kumwabudu Mungu. Hii ndiyo athari ya kazi ya Roho Mtakatifu, na ni kinyume kabisa cha kazi ya pepo wabaya.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)
Hapa chini, hebu tuangalie baadhi ya utofauti mwingine waziwazi kati ya kazi mbalimbali za pepo wabaya na kazi ya Roho Mtakatifu, na namna ambavyo zinaonyeshwa kwa njia mahususi. Roho Mtakatifu huwachagua watu wanaofuatilia ukweli, na walio na dhamiri na mwelekeo, na wanaomiliki uadilifu. Hawa ndio aina ya watu ambao Roho Mtakatifu hufanya kazi ndani yao. Pepo wabaya huchagua watu ambao ni wajanja na wa kipuuzi, wasiopenda ukweli, na wasio na dhamiri wala mwelekeo. Watu kama hao ndio pepo wabaya hufanya kazi ndani yao. Ni nini tunachoona tunapolinganisha wale waliochaguliwa kwa kazi ya Roho Mtakatifu, na wale waliochaguliwa kwa kazi ile ya pepo wabaya? Tunaweza kuona kwamba Mungu ni mtakatifu, na mwenye haki, kwamba wale wanaochaguliwa na Mungu huutafuta ukweli, na wanayo dhamiri na mwelekeo, kwamba wanao uadilifu na wanapenda kile ambacho ni haki. Wale wanaochaguliwa na pepo wabaya ni wajanja, ni wachoyo na wenye dharau, hawaupendi ukweli, hawana dhamiri na mwelekeo, na hawautafuti ukweli. Pepo wabaya huchagua tu mambo mabaya na wale watu ambao si wa kweli, ambapo tunaona ya kwamba pepo wabaya wanapenda uovu na giza, kwamba wanawakimbia wale wanaoutafuta ukweli, na ni wepesi wa kuwamiliki wale ambao wako kombo na ni wajanja, wale ambao wanavutiwa na udhalimu, na wanaorogwa kwa urahisi. Wale ambao pepo wabaya huchagua kufanyia kazi ndani yao hawawezi kuokolewa, na wanaondolewa na Mungu. Ni lini, na ni katika mazingira gani, ndipo pepo wabaya hufanya kazi? Wao hufanya kazi wakati watu wamesonga mbali na Mungu na kuasi dhidi ya Mungu. Kazi ya pepo wabaya huwaroga watu, na hufanya hivyo kwa kuchukua fursa ile wanapotenda dhambi. Wakati watu wako katika hali yao dhaifu zaidi, hasa wanapokuwa katika maumivu makuu ndani ya mioyo yao, wakati wanapohisi vibaya na wakiwa wamechanganyikiwa, pepo mbaya huchukua fursa hii kujiingiza ndani polepole ili kuwaroga na kuwapotosha, kuleta kutoelewana kati yao na Mungu. Kunao wakati wa kazi ya Roho Mtakatifu: Wakati watu wanapomwita Mungu, wakati mioyo yao inapomgeukia Mungu, wanapomhitaji Mungu, wanapotubu kwa Mungu, na wanapoutafuta ukweli, basi ndipo Roho Mtakatifu huanza kufanya kazi ndani yao. Tazama namna ambavyo kila dhana ya kazi ya Roho Mtakatifu ilivyo ili kumwokoa mwanadamu, namna Anavyotafuta fursa za kumwokoa mwanadamu, ilhali pepo wabaya hutafuta fursa za kuwapotosha na kuwalaghai watu. Pepo wabaya wanayo dharau na ni waovu, ni wenye kudhuru kwa siri na wabaya, kila kitu wanachofanya kinalenga katika kumpotosha mwanadamu, na kumdhuru mwanadamu, na kumteketeza yeye. Wakati watu wanapohitaji msaada, wanapomtafuta Mungu kwa dharura, wanapohitaji wokovu wa Mungu, na wanapotaka kusonga karibu na Mungu ndani ya mioyo yao, Roho Mtakatifu hujitokeza kwao na kufanya kazi ya wokovu. Mungu ni upendo, na pepo wabaya ni chuki—hili liko wazi kwako, sivyo? Kile tu ambacho pepo wabaya hufanya ni ili kuwezesha kumteketeza na kumpotosha mwanadamu, na kile tu ambacho Roho Mtakatifu hufanya ni kwa upendo na wokovu wa mwanadamu. Athari ya kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwatakasa watu, kuwaokoa dhidi ya kupotoka kwao, kuwaruhusu kujijua na kumjua Shetani, kuweza kuasi dhidi ya Shetani, kuweza kuufuatilia ukweli, na hatimaye kuishi kwa kudhihirisha mfanano wa mwanadamu. Pepo wabaya hupotosha, hutia najisi, na kuwafunga watu, huwaweka ndani zaidi ya dhambi, na kuwasababishia maumivu makubwa zaidi katika maisha yao, na hivyo wakati pepo wabaya wanapofanya kazi ndani ya watu, watu hao wamo hatarini; hatimaye, wanateketezwa na Shetani, jambo ambalo ni matokeo ya kazi ya pepo wabaya. Athari ya kazi ya Roho Mtakatifu ni kuweza hatimaye kuwaokoa watu, kuwafanya kuishi kwa kudhihirisha maisha halisi, kuwa huru na kukombolewa kabisa, na kupokea baraka za Mungu. Tazama: Pepo wabaya humweka mwanadamu katika giza, humpeleka kwenye shimo la kuzimu; Roho Mtakatifu humchukua mwanadamu kutoka kwenye giza, na kumpeleka kwenye mwangaza, na hadi kwenye uhuru. Kazi ya Roho Mtakatifu huwapa watu nuru na kuwaongoza watu, Huwapa fursa mbalimbali, na wanapokuwa wanyonge na dhambi Yeye huwapa faraja. Huwaruhusu watu kujijua, huwaruhusu kuufuatilia ukweli, na Halazimishi watu kufanya mambo, lakini Huwaacha kujichagulia njia yao wao wenyewe, na hatimaye Huwapeleka kwenye mwangaza. Pepo wabaya huwalazimisha watu kufanya mambo na kuwaamrisha hapa na pale. Kila kitu wanachosema ni uongo na kinawaroga watu, kuwadanganya na kuwafunga; pepo wabaya hawawapatii watu uhuru, hawawaruhusu kuchagua, huwalazimisha kufuata barabara ya maangamio, na hatimaye kuwaingiza ndani ya dhambi zaidi na zaidi, na kuwasababishia kifo. Hebu tazama watu hao waovu, wale watu waovu: Wanawakokota wengine hadi kwenye uharibifu, wanawavuta kwenye uhalifu, na kuwavuta kwa ghafla kwenye maeneo ya kuchezea kamari. Hatimaye, baada ya wao kuziharibu familia za watu na kuwafarakanisha na dunia, wanafurahi, kazi yao imekamilika, na wametimiza nia yao. Je, hawa ni mashetani, sivyo? Ilhali wale ambao ni wazuri kwa kweli na wanamcha Mungu wanawaongoza watu kuwa karibu zaidi na Mungu, na kuwaongoza katika imani ya Mungu, katika ufahamu wa ukweli, katika kuyafuatilia maisha halisi, na hatimaye kuwafanya kuishi kwa kudhihirisha mfanano wa mwanadamu. Utofautishi kati ya mambo haya mazuri na mabaya ni wazi vipi! Katika kulinganisha kanuni, mbinu, na athari ya mwisho ya kazi ya Roho Mtakatifu na ile ya pepo wabaya, tunaona kwamba Mungu humwokoa mwanadamu, humpenda mwanadamu, na humpa mwanadamu ukweli, kwamba Yeye humchukua mwanadamu na kumweka kwenye mwangaza, na hatimaye humruhusu mwanadamu kubarikiwa na kuwa mtu halisi na kuishi kwa kudhihirisha maisha ya ukweli. Shetani humpotosha mwanadamu, humfunga mwanadamu, hujaribu kumteketeza mwanadamu, na hatimaye humwongoza mwanadamu katika kuteseka milele na kuangamia. Kupitia kujua kazi ya Roho Mtakatifu, tunaweza kutambua kazi ya pepo wabaya na kuujua ukweli wa upotoshwaji wa mwanadamu na Shetani. Leo, katika imani yetu kwa Mungu tunafahamu kile tunachofaa kufuatilia, kwamba Mungu ni mzuri, na kwamba tunafaa kumjua Mungu, kumwabudu Mungu, na kumtii Mungu. Tunayo malengo katika maisha yetu, na tunalo tumaini la wokovu. Hizi ndizo athari za kazi ya Roho Mtakatifu. Leo, kama ungeulizwa kusema Shetani ni nini, ungeweza kusema? Tabia potovu ya Shetani inaonyeshwa kwa njia gani? Tabia ya Shetani ni yenye maovu, yenye kudhuru kwa siri, yenye makosa, mbovu, yenye dharau, yenye kushikilia maovu yote, na yenye sumu kabisa. Kila kitu ambacho Mungu anacho na Alicho ni nini? Ni hali ya kuwa mwenye haki, utakatifu, heshima, kudura, hekima, na rehema na upendo. Ile hisia ambayo Shetani huwapatia watu ni ya kuchukiza na iliyolaaniwa. Ile hisia ambayo Mungu huwapatia watu ni ya kukaribishwa, uzuri na kuheshimiwa.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)
Ni nini athari ya kazi ya Roho Mtakatifu kwa mwanadamu? Humruhusu mwanadamu kuyaelewa maneno ya Mungu, na ukweli, na humruhusu mwanadamu kumjua Mungu na kujijua. Ukweli unao athari maradufu. Kwa upande mmoja, kuufahamu ukweli huwapatia watu maarifa ya Mungu, kwani ukweli ndio kiini cha maisha ya Mungu, ni kile Mungu anacho na Alicho, ni uhalisi wa mambo mazuri, na unawakilisha tabia na maisha ya Mungu—na hivyo basi ni sahihi kabisa kusema kwamba, kwa kuuelewa ukweli, tunafaidi ufahamu fulani wa Mungu. Wakati uo huo, ukweli unaweka pia wazi kupotoka kwetu, na hivyo basi wale wote wanaouelewa ukweli wanayo maarifa ya kweli kujihusu, na wameona wazi kabisa picha yao ya kweli na picha ya kweli ya Shetani. Kila kitu kinawekwa wazi kwa ukweli. Ni nini athari ya ufahamu wa ukweli kupitia kazi ya Roho Mtakatifu? Kwa upande mmoja, tunakijua kiini chetu potovu, tunamwona kwamba mwanadamu ni maskini, wa kuhurumiwa, kipofu, aliye na uchi, aliyepotoka, mwovu, mchoyo na mwenye dharau, kwamba hana mfanano hata kidogo wa mwanadamu wa kweli, kwamba hayuko tofauti hata kidogo na Shetani, kwamba asili yake na kiini chake vyote viko sawa na Shetani. Je, hii si athari ya ufahamu wa ukweli? Hakuna chochote ambacho si sahihi kuhusu haya. Isitoshe, kwa mtazamo huu tuko wazi kabisa kuhusu athari za kazi ya Roho Mtakatifu. Kazi ya Roho Mtakatifu inayo pia athari nyingine nyingi. Kazi ya Roho Mtakatifu inaweza kuwapa watu imani ya kweli: Kila mojawapo ya maombi yetu kwa Mungu hutufanya kuhisi kwamba imani yetu kwa Mungu imeongezeka, na kwamba ni kweli zaidi. … Si ukweli hata kidogo kusema kwamba kunazo sehemu nyingi katika kazi ya Roho Mtakatifu, na mitazamo mingi ya athari zake. … kazi ya Roho Mtakatifu hutupatia maarifa ya kweli ya tabia ya Mungu, ya kudura na hekima ya Mungu, ya uchanganuzi Wake wa kina wa mioyo yetu, na hutupatia maarifa ya matendo ya ajabu na hali isiyofikirika kuhusu Mungu. Hivyo, pia, ndivyo inavyoturuhusu kujua na kushikilia kudura ya Mungu na utawala wake dhidi ya vyote.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)
Wale ambao pepo wabaya hufanya kazi ndani yao hugeuka na kuwa wabaya na wazi na wenye kufanya jeuri wakati wanapoongea na kuwaambia watu ni nini cha kufanya. Baadhi yao hata hukiuka tabia njema na maadili ya ubinadamu wa kawaida. Maneno yao na vitendo vyao huroga na kuingilia kati watu, asili ya maneno hayo na vitendo hivyo ni mbovu na ya kuchukiza, na wanapotosha watu, na kuwadhuru watu, na hawana manufaa yoyote kwao. Punde tu pepo mbaya anapoonekana ndani ya mtu, wanahisi woga na wasiwasi, na kunakuwa na dharura kuu katika vitendo vyao, ni kana kwamba wanalipuka kwa kutokuwa wastahimilivu. Kuonekana kwake huwafanya watu kuhisi hasa kwa njia isiyo ya kawaida, na hakuna manufaa yoyote hata kidogo kwa wengine. Maonyesho makuu ya kazi ya pepo wabaya: Onyesho la kwanza ni kuwaelekeza watu kufanya hivi au vile, kuwaambia kufanya mambo, au kuwaelekeza kuongea unabii wa uongo. Onyesho la pili ni kuongea kwa mbinu ile ijulikanayo kama ya "ndimi" ambayo hakuna anayeielewa; hata wasemaji wenyewe hawawezi kuelewa kile wanachosema, na baadhi yao wanaweza "kuifasiri." Onyesho la tatu ni pale ambapo watu siku zote wanaupokea ufunuo, unaofanyika kwa uradidi fulani. Kwa wakati mmoja wataelekezwa kufanya kitu kimoja, na kwa wakati mwingine wataambiwa kufanya kitu kingine, na wanaishi katika wasiwasi usioisha. Onyesho la nne: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao wanayo hamu ya kufanya hiki au kile, na hawawezi kusubiri—licha ya kama kitu hicho kinakubaliwa katika mazingira yao au la. Huwa hata wanatoka nje kwenye giza la usiku; mwenendo wao si wa kawaida kamwe. Onyesho la tano: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao huwa hasa wenye majivuno na kiburi, kila kitu wanachosema ni cha kushusha hadhi na kuamrisha, hawawezi kuuongea ukweli wowote, anawaacha watu wakiwa wamekasirika, na kuwalazimisha watu kuingia kwenye taabu kama pepo. Onyesho la sita: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao hawana ufahamu kiasi kidogo cha mipangilio kutoka juu, isitoshe hawaelewi kanuni za kazi; wanamkenulia Mungu, wanajaribu kuwadanganya watu, na matendo yao mabaya yanatatiza mpangilio wa kawaida wa kanisa. Onyesho la saba: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao mara nyingi hujifanya kuwa watu wengine bila sababu, au vinginevyo wametumwa na mtu, kuwafanya watu kuyasikiliza maneno yao, na hakuna anayeweza kujua namna walivyofikia hapo. Onyesho la nane: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao mara nyingi hawana urazini, na hawauelewi ukweli; kwa kawaida, wanakosa welekevu wa kuelewa, na hawana kule kupewa nuru na Roho Mtakatifu. Watu hugundua kwamba kile wanachoelewa hasa si cha kawaida, na si sahihi kabisa. Onyesho la tisa: watu ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao ni wenye makuu kabisa na wasio na urazini, hawamtukuzi Mungu wala kumtolea ushuhuda kamwe, hawawezi kuuongea ukweli wowote, na kile wanachofanya na kusema tu huwa kinawashambulia watu, kinawafunga, na kuwawekea mipaka, mpaka pale ambapo mioyo yao imeshughulikiwa, na wao kupigwa na kugeuzwa kuwa wabaya na wasioweza kujiokoa, huku nao wakiwa na furaha kisirisiri—ambayo ndiyo nia kuu ya kazi ya pepo wabaya. Onyesho la kumi: watu ambao wamepagawa na pepo wabaya—maisha yao yana kasoro kabisa, mtazamo wao mkali, na maneno yao hasa hayana urafiki, ni kana kwamba wao ni pepo ambaye ameingia ulimwenguni humu. Hakuna nidhamu katika maisha yao ya kila siku, hawana uthabiti kabisa, wao hawatabiriki kama vile wale wanyama wasiofugwa, wanyama mwitu, na watu wanawaona kuwa wanaweza kupingika kabisa. Hayo ndiyo maonyesho ya watu waliofungwa na mashetani. Watu ambao wamepagawa na pepo wabaya mara nyingi hasa wanakuwa wenye chuki na kujitenga na wale ambao Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yao na wanaoweza kuuongea ukweli. Ndivyo inavyokuwa mara nyingi kwamba watu wanapokuwa bora zaidi, ndipo wanapotaka kuwashambulia na kuwashutumu, ilhali watu wanapokosa mwelekeo na kuchanganyikiwa zaidi, ndipo wanapofanya kadri wanachoweza kuwalaghai na kuwavisha kilemba cha ukoka, na hasa wao kuwa radhi kujihusisha nao. Kazi ya pepo wabaya hugeuza nyeusi ikawa nyeupe, na kuyafanya mazuri kuwa mabaya na mabaya kuwa mazuri. Hayo ndiyo matendo ya pepo wabaya.
kutoka kwa "Maonyesho Makuu ya Kazi ya Pepo Wabaya" katika Ushirikiano Kutoka kwa wa Juu
Roho yoyote ambayo kazi yake inajionyesha katika hali isiyo ya ulimwenguni humu ni pepo mbaya, na kazi na matamko ya roho yoyote inayotekeleza kazi isiyo ya ulimwenguni humu ndani ya watu ni kazi ya pepo mbaya; mbinu hizi zote ndizo ambazo pepo wabaya hufanya kazi na si za kawaida na za humu ulimwenguni, na zinaonyeshwa kimsingi kwa njia sita zifuatazo:
1. Udhibiti wa moja kwa moja wa uneni wa watu, jambo ambalo linaonyesha waziwazi kwamba pepo mbaya anazungumza, na wala si watu wenyewe wanaozungumza kwa kawaida;
2. Hisia kwamba pepo mbaya anawaelekeza watu na kuwaamuru kufanya hiki na kile;
3. Watu ambao, wakati wakiwa kwenye chumba, wanaweza kujua wakati mtu yuko karibu kuingia ndani;
4. Watu ambao mara nyingi wanazisikia sauti zikiwazungumzia na ambazo wengine hawawezi kuzisikia;
5. Watu ambao wanaweza kuona na kusikia mambo ambayo wengine hawawezi;
6. Watu ambao siku zote wanafadhaishwa, na wanajizungumzia wenyewe, na hawawezi kuwa katika mazungumzo ya kawaida au utangamano na watu.
Wale wote ambao pepo mbaya anafanya kazi ndani yao bila kuepukika wanayo maonyesho haya sita. Wao hawana urazini, siku zote wako katika hali ya taharuki, hawawezi kutangamana na watu kwa njia ya kawaida, ni kana kwamba wao hawashawishiki kwa lolote lile, na kuna jambo lililojitenga na lisilo lao. Watu kama hao wamepagawa na pepo mbaya au wanaye pepo mbaya anayefanya kazi ndani yao, na kazi yote ya pepo wabaya inajionyesha na si ya ulimwenguni humu. Hii ndiyo kazi inayotambulika kwa haraka zaidi kuhusu pepo wabaya. Wakati pepo mbaya anapompagaa mtu, anacheza nao kiasi cha kwamba wanaathirika kabisa. Wanakosa urazini, kama zuzu, hali ambayo inathibitisha kwamba kiini cha mambo ni kuwa, pepo wabaya ni pepo waovu wanaopotosha na kuteketeza watu. Matamko ya pepo wabaya ni rahisi kuyatambua: Matamko yao yanaonyesha kikamilifu kiini chao cha uovu, yapo palepale, yamevurugika, na yananuka, yanarishai harufu ya kifo. Kwa watu walio na uhodari mzuri, maneno ya pepo wabaya huwafanya kuhisi utupu na kutovutiwa, yasiyorekebisha maadili, yasiyo na chochote ila uongo na maneno yasiyo na maana, wanahisi wakiwa wamevurugika na wanaona ugumu kuelewa yote haya, kama zigo la upuuzi. Huu ni baadhi ya upuuzi unaotambulika kwa haraka zaidi kuhusu pepo wabaya. Kuwaroga watu, baadhi ya wale pepo wabaya wa "kiwango cha juu" hujifanya kuwa Mungu au Kristo wanapoongea, huku wengine wakijifanya kuwa malaika au watu maarufu. Wanapoongea, pepo hawa wabaya ni stadi katika kuiga maneno au kauli fulani za Mungu, au sauti ya Mungu, na watu wasiouelewa ukweli wanadanganywa kwa urahisi na pepo kama hawa wabaya wa "kiwango cha juu." Watu wa Mungu waliochaguliwa lazima wawe wazi kwamba, kiini cha mambo ni kwamba, pepo wabaya ni waovu na wasio na aibu, na hata kama wao ni pepo wabaya wa "kiwango cha juu," wao hawana ukweli kabisa. Pepo wabaya, zaidi ya yote, ni pepo wabaya, kiini cha pepo wabaya ni uovu, na wenye sampuli moja na Shetani.
kutoka kwa "Jinsi ya Kutambua Upumbavu na Uongo wa Roho Waovu, Makristo wa Uongo, na Wapinga Kristo" katika Kumbukumbu za Kihistoria za Ushirika na Mipangilio ya Kazi ya Kanisa (II)
Kila kitu ambacho pepo wabaya hufanya si cha ulimwenguni humu kabisa, wao huelekeza moja kwa moja watu kufanya hiki au kile, huwaamuru moja kwa moja kufanya hiki na kile, huwalazimisha kwa njia ya moja kwa moja kufanya mambo—haya ndiyo maonyesho ya kazi ya pepo wabaya. Kazi ya Roho Mtakatifu haijawahi kuwalazimisha watu kufanya hiki au kile, haijawahi kuwaamuru watu huku na kule, haijawahi kukosa kuwa ya ulimwenguni humu, haijawahi kutumia mbinu zisizo za ulimwenguni humu kuwaelekeza watu kufanya mambo, siku zote imefichwa ndani kabisa ya watu, na inawagusa kupitia kwa dhamiri yao ili kuwafanya kuuelewa ukweli na maneno ya Mungu, na baadaye hutumia dhamiri kuwafanya kuuweka ukweli ule katika matendo. Hii ndiyo mbinu ambayo Roho Mtakatifu hufanyia kazi. Roho Mtakatifu hajawahi kuwalazimisha wala kuwashurutisha watu, Hajawahi kufanya chochote kisicho cha ulimwenguni humu au chenye maonyesho, na Haelekezi watu waziwazi. Tunajua nini kutoka kwa haya? Tunajua kwamba kazi ya Roho Mtakatifu ni nyenyekevu na fiche, na hasa fiche, na hakuna yoyote yake imefichuliwa. Mungu ni mwenye kudura na anashikilia utawala dhidi ya vitu vyote, lakini Roho Mtakatifu hamwambii mwanadamu kwa njia ya moja kwa moja, "Aisee, unafaa kufanya hivi au vile." Roho Mtakatifu hajawahi kuchukua hatua namna hii; Yeye hukugusa, kwa kutumia upendo Yeye hukugusa, na Yeye ni mtulivu sana, kiasi cha kwamba huhisi kama mtu anakugusa—lakini kwenye kina cha moyo wako unahisi kwamba unafaa kuchukua hatua kwa njia fulani, na kwamba ni sahihi na bora kufanya hivyo. Tazama namna ambavyo Mungu alivyo mzuri! Tazama tena sura mbovu na ya kuhurumiwa ya wale waliopagawa na pepo wabaya, tazama ambavyo, pindi wanapokutana na watu, wanasema, "Leo roho amenielekeza kusema hivi, ameniambia kufanya vile, amenifanya kufanya hivi," angalia namna ambavyo wakati mwingine wanavyoamka kwenye usiku wa giza kueneza injili, au kuomba, au kusema namna ambavyo wameguswa na lazima watimize wajibu wao. Tazama namna, punde watu wanapofungwa na pepo mbaya, yeye huwasababishia mateso mabaya, na kuwafanya kusambaratika, tazama namna ambavyo hawajui ni lini watakula au kufanya mambo, namna ambavyo maisha yao yamebadilika na kuwa kombo. Wakati ambapo pepo wabaya wanafanya kazi ndani ya watu, wao huwazungusha huku na kule, na kuwaacha wakiwa wamechoka na hoi. Hatimaye, wanaambulia patupu: Hakuna mabadiliko katika tabia yao ya maisha, wangali bado wamepotoka kama walivyokuwa awali, wale ambao kwa kawaida walikuwa na majivuno na makuu wangali bado na majivuno na makuu, na wale waliokuwa wajanja na wakujitia mapuuza wangali wajanja na walewale wa kujitia mapuuza. Kazi ya pepo wabaya huwapotosha watu, na kuwaacha wakiwa si wa kawaida kiakili. Kutoka kwenye utaratibu wa utendaji wa pepo wabaya, tunaona tu namna ambavyo wana dharau, uovu, mapuuza, na ujinga. Hafanyi chochote ila kuwanyanyasa na kuwapotosha watu, kwa sababu ya haya wanachukiwa na kulaaniwa na watu, wanaosema kwamba wao ni wabaya. Hivyo, kazi ya pepo wabaya inamwakilisha Shetani—hakuna kosa katika haya. Yeyote aliyewaona watu ambao pepo wabaya hufanya kazi ndani yao, au wale waliopagawa na Shetani, anajua tu namna wanavyochukiza, walivyo na mapuuza, uovu, na walivyojaa upotovu. Je, mnayaona haya? Je, mnayaona baadhi yake, sivyo? Je, mmeona kwamba pepo wabaya wanaumiliki ukweli? Je, pepo wabaya wanao upendo wowote kwa wanadamu? Kutoka kwenye kazi ya pepo wabaya, inaweza kuonekana kwamba hawana ukweli hata kidogo, na kwamba asili yao ni ya uovu kabisa. Baada ya kuona namna ambavyo pepo wabaya wanavyowapotosha watu, umeona namna ambavyo Shetani hupotosha watu—ni ukweli kabisa. Kwa sababu pepo wote wabaya wanashirikiana na Shetani, kwani wote wanamfuata Shetani, na ndio washiriki, marafiki, na washirikishi wa Shetani, wamekuwa na Shetani tangu hapo zama za kale. Shetani aliwaongoza pepo hawa wote wabaya katika kuasi dhidi ya Mungu na akaangushwa hapa ulimwenguni. Je, pepo mbaya angeweza—pepo mbaya asiye na ukweli na mwenye kuasi kabisa Mungu katika asili yake—kuuleta ukweli wowote kwa mtu anapompagaa? Anaweza kuyaleta mabadiliko katika tabia zao? Bila shaka, la.
kutoka kwa "Kujua Kazi ya Roho Mtakatifu Kuna Umuhimu Mkubwa kwa Wokovu wa Mwanadamu" katika Mahubiri na Ushirika juu ya Kuingia Katika Maisha (II)
Kujua zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni