Alhamisi, 28 Februari 2019

Muziki wa Injili "Maneno Ya Mungu Ni Ukweli Usiobadilika Milele"

Muziki wa Injili "Maneno Ya Mungu Ni Ukweli Usiobadilika Milele"

Maneno ya Mungu ni ukweli, usiobadilika milele.
Mungu ndiye mpaji wa uzima, na kiongozi pekee wa mwanadamu.
Thamani na maana ya maneno Yake yanaamuliwa na kiini chao,
sio kama mwanadamu anayakubali au kuyatambua.
Hata kama hakuna mwanadamu ulimwenguni anayapokea maneno Yake,
thamani yao na usaidizi kwa mwanadamu hayapimiki.
Maneno ya Mungu ni ukweli, usiobadilika milele.
Mungu ndiye mpaji wa uzima, na kiongozi pekee wa mwanadamu.

Jumatano, 27 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku”

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku”

Mwenyezi Mungu anasema, “Kuanzia leo, Mungu ataweza kuwafanya watu wasiokuwa na fikira za kidini kuwa watimilifu kwa njia rasmi, ambao wako tayari kuweka pembeni nafsi zao za kale, na ambao wanamtii tu Mungu, pamoja na kuwafanya kuwa watimilifu wale wanaotamani neno la Mungu. Watu hawa wanafaa kusimama na kumhudumia Mungu. Kwake Mungu kunayo na hekima nyingi na isiyoisha. Kazi yake ya kustaajabisha na matamshi yake yenye thamani ni vitu ambavyo vipo ili watu wengi zaidi kuweza kufurahia.

Jumanne, 26 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Ahadi kwa Wale Ambao Wamekamilishwa”

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Ahadi kwa Wale Ambao Wamekamilishwa”

Mwenyezi Mungu anasema, “Wale watakaokamilishwa na Mungu ni wale watakaopokea baraka za Mungu na urithi Wake. Yaani, wanasikia na kuelewa kile Mungu Alicho nacho na Alicho, ili kiwe kile ambacho walicho nacho ndani yao; wanayo maneno yote ya Mungu ndani yao; haijalishi ni vipi nafsi ya Mungu ilivyo, mnaweza kusikia na kuelewa kila kitu Anachokuambia vile kilivyo, na hivyo kuishi kwa kudhihirisha ukweli. Huyu ndiye aina ya binadamu aliyekamilishwa na Mungu na aliyepatwa na Mungu.”

Jumatatu, 25 Februari 2019

Ufafanuzi wa Mafumbo ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima | Sura ya 17

Sura ya 17

Mwenyezi Mungu alisema: Kwa kweli, maneno yote kutoka katika kinywa cha Mungu ni mambo ambayo wanadamu hawayajui; yote ni lugha ambayo watu hawajasikia, kwa hiyo inaweza kusemwa hivi: Maneno ya Mungu yenyewe ni siri. Watu wengi kwa kutojua wanaamini kwamba ni mambo tu ambayo watu hawawezi kutimiza kimawazo, mambo ya mbinguni ambayo Mungu anawawezesha watu kuyajua sasa, au ukweli kuhusu kile Mungu anachofanya katika ulimwengu wa kiroho ni siri.

Jumapili, 24 Februari 2019

Swahili Christian Skit "Mipaka ya Meya wa Kijiji" | Why Is There No Religious Freedom in China?

Mchezo mfupi Mipaka ya Meya wa Kijiji inaeleza hadithi ya kweli ya mume na mke Wakristo ambao wanalazimishwa kutoroka kwa sababu ya mateso ya serilaki ya CCP. Mkristo Liu Ming'en anahukumiwa na CCP miaka saba gerezani kwa kuamini katika Mungu. Hata baada ya kuachiliwa kutoka gerezani, anabakia kuwa wakulengwa na uchunguzi mkali wa CCP. Meya wa kijiji anatumia mfumo wa wajibu wa kaya-tano , kamera za usalama, ziara za nyumba, na njia nyingine kumzuia Liu Ming'en na mkewe kuamini katika Mungu, lakini hakuna inayoleta na matokeo yanayotakiwa.

Jumamosi, 23 Februari 2019

Wimbo wa Injili "Kiini cha Kristo Ni Mungu" | Differences Between the True Christ and False Christs

Wimbo wa Injili "Kiini cha Kristo Ni Mungu" | Differences Between the True Christ and False Christs

Mungu anayekuwa mwili anaitwa Kristo,
na hivyo Kristo anayeweza kuwapa watu ukweli anaitwa Mungu.
Si kupita kiasi kusema hivyo,
kwani Ana kiini cha Mungu, Ana tabia ya Mungu na hekima katika kazi Yake,
ambayo haifikiwi na mwanadamu.
Wale wanaojiita Kristo wenyewe ilhali hawawezi kufanya kazi ya Mungu ni wadanganyifu.
Wanaojifanya kuwa Kristo hatimaye wataanguka,
ingawaje wanadai kuwa Kristo,
hawana kiini chochote cha Kristo.

Ijumaa, 22 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu” (Sehemu ya Kwanza)

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu” (Sehemu ya Kwanza)

Mwenyezi Mungu anasema, "Kazi Aifanyayo Mungu ni kwa ajili ya wanadamu wote na mawazo Yake daima ni mema. Kwa mwanadamu, kwa hivyo, kazi ya Mungu na mawazo ya Mungu kwa mwanadamu (yaani mapenzi ya Mungu) ni “maono” ambayo yanafaa kutambuliwa na mwanadamu. Maono kama hayo pia ni usimamizi wa Mungu, na kazi ambayo haiwezi kufanywa na mwanadamu. Mahitaji ambayo Mungu anatarajia kutoka kwa mwanadamu wakati wa kazi Yake, wakati uo huo, yanaitwa “vitendo” vya mwanadamu.

Alhamisi, 21 Februari 2019

Ufafanuzi wa Mafumbo ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima | Sura ya 16

Sura ya 16

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa watu, Mungu ni mkuu mno, mwenye utele mno, wa ajabu mno, Asiyeeleweka mno; machoni pao, maneno ya Mungu hupaa juu, na huonekana kama kazi bora sana ya ulimwengu. Lakini kwa vile watu wana kasoro nyingi sana, na akili zao ni za kawaida sana, na, zaidi ya hayo, kwa kuwa uwezo wao wa kukubali ni haba mno, bila kujali vile Mungu hunena maneno Yake kwa dhahiri, wanabaki palepale bila kutikisika, kana kwamba wana ugonjwa wa akili.

Jumatano, 20 Februari 2019

Wimbo wa Maneno ya Mungu | "Kusudi la Kazi ya Mungu la Usimamizi" | The True Love of God for Man

Wimbo wa Maneno ya Mungu | "Kusudi la Kazi ya Mungu la Usimamizi" | The True Love of God for Man

Mungu ana mpango wa usimamizi wa miaka 6,000,
uliyogawanywa katika hatua tatu, kila moja inaitwa enzi.
Kwanza ni Enzi ya Sheria, kisha Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme ni awamu ya mwisho.
Ingawa kazi ya Mungu ni tofauti katika kila moja,
yote inalingana na kile ambacho binadamu wanahitaji,
ama hasa inalingana na ujanja ambao Shetani anatumia, anapopigana na Yeye.
Kusudi la Kazi ya Mungu ni kumshinda Shetani,
kufunua hekima ya Mungu na ukuu,
na kufichua ujanja wote wa Shetani,
hivyo kumwokoa mwanadamu kutoka kwa utawala wake,
hivyo kumwokoa mwanadamu kutoka kwa utawala wake.

Jumanne, 19 Februari 2019

Swahili Christian Skit | "Baba Yangu, Mchungaji" | A Debate on the Bible in a Family

Chi Shou, mchungaji wa dini ambaye amekuwa muumini wa Bwana kwa miaka arubaini, daima ameshikilia mitazamo kwamba "maneno na kazi yote ya Bwana yako ndani ya Biblia," na kwamba "imani katika Bwana haiwezi kuacha Biblia, na kuiamini Biblia humaanisha kumwamini Bwana." Inapojulikana kwamba binti yake ameikubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho, anafanya mpango na mke wake kumkomesha. Katika siku hii, binti yao anarudi nyumbani kushuhudia injili ya kurudi kwa Bwana, na mjadala mkali, mcheshi, ilhali mzito wa familia unatokea ...
Kuhusu Sisi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatatu, 18 Februari 2019

Maonyesho ya Mungu | “Wewe U Mwaminifu kwa Nani?” (Official video)

Maonyesho ya Mungu | “Wewe U Mwaminifu kwa Nani?” (Official video)

Mwenyezi Mungu anasema, “Mmekuwa wafuasi Wangu kwa miaka mingi sana, lakini hamjawahi kunionesha hata chembe ya uaminifu. Badala yake mmekuwa mkizunguka kwa watu mnaowapenda na vitu vinavyowapendeza sana, na kuviweka karibu na mioyo yenu na havijawahi kuachwa, wakati wowote, mahali popote. ... Mnajiweka wenyewe katika shughuli ambazo mnazipenda: Wengine ni waaminifu kwa watoto, wengine kwa waume, wake, utajiri, kazi, wenye vyeo, umaarufu, au wanawake.

Jumapili, 17 Februari 2019

Mchezo Mfupi wa Kuchekesha | "Njama za Polisi" (Swahili Subtitles)

Ili kuondoa imani za dini, serikali ya CCP ambayo inakana Mungu mara kwa mara inatumia mikakati ya kuchunguza Wakristo kama vile kuendesha uchunguzi wa siri na kufuatilia ili kuwafutilia mbali wote. Kichekesho cha Njama za Polisi kinahusu ushirikiano wa maafisa waovu wa CCP katika sura fiche na ofisa msaidizi, punda anayevaa ngozi ya simba, anayeendesha ufuatiliaji wa siri wa kuwatia mbaroni Wakristo wanaokusanyika kwenye nyumba ya Zhao Yuzhi. Je, Zhao Yuzhi na familia yake watashughulikiaje njama ovu za polisi wa Kichina? Je, ni shida gani zitakazowakumba wao?

Jumamosi, 16 Februari 2019

Wimbo wa Maneno ya Mungu | "Jinsi ya Kujua Kuonekana na Kazi ya Kristo wa Siku za Mwisho"

Wimbo wa Maneno ya Mungu | "Jinsi ya Kujua Kuonekana na Kazi ya Kristo wa Siku za Mwisho"

I
Mwili wa Mungu utajumlisha kiini cha Mungu na maonyesho Yake.
Atakapofanywa mwili, Ataleta matunda ya kazi Aliyopewa
ajidhihirishe na Alete Ukweli kwa wote,
awape uhai na awaonyeshe njia.
Mwili wowote usiokuwa na dutu Yake sio Mwili wa Mungu.

Ijumaa, 15 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa “Maonyo Matatu” | How to Be a Loyal Servant of God

Mwenyezi Mungu anasema, “Kama muumini wa Mungu, hufai kuwa watiifu kwa yeyote mwingine isipokuwa Yeye katika mambo yote na mjilinganishe na moyo Wake katika mambo yote. Hata hivyo, ingawa wote huelewa mafundisho haya, ukweli huu wa kimsingi ulio wazi kabisa kwa binadamu hauwezi kuonekana kuwa kujumuishwa kwao kikamilifu, kutokana na ugumu wao, kama vile hali yao ya kutojua, upuzi, au ufisadi.

Alhamisi, 14 Februari 2019

Filamu za Kikristo 2018 | "Kumbukumbu Chungu" | Welcoming the Return of the Lord in Judgement

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Filamu za KikristoFilamu za Kikristo 2018 | "Kumbukumbu Chungu" | Welcoming the Return of the Lord in Judgement

Fan Guoyi alikuwa mzee wa kanisa la nyumba kule Uchina. Wakati wa zaidi ya miaka ishirini ya huduma, siku zote alimwiga Paulo, na kufanya kazi kwa bidii na akamtumikia Bwana kwa shauku kubwa. Aidha, alisadiki kabisa kwamba katika kufuata imani yake kwa njia hii, alikuwa akitenda mapenzi ya Baba wa mbinguni, na kwamba wakati Bwana angerudi, angenyakuliwa kwa hakika na kuenda kwenye ufalme wa mbinguni. Hata hivyo, wakati wokovu wa Mwenyezi Mungu wa siku za mwisho ulipomjia, alishikilia kwa dhana zake.

Jumatano, 13 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu”

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu”

Mwenyezi Mungu anasema, “Hata ingawa fikira za mwanadamu hakika haziwezi kupuuzwa, haikubaliki hata zaidi kwa mwanadamu kubadilisha kiini cha Kristo. Nyinyi mnamchukua Kristo kama asiyekufa au mhenga, lakini hakuna yeyote anayemchukua Kristo kama binadamu wa nyama na mwili aliye na kiini kitakatifu. Kwa hivyo, wengi wa wale ambao wanatamani usiku na mchana kumwona Mungu ni hasa maadui wa Mungu na hawapatani na Mungu. Je, haya si makosa kwa upande wa mwanadamu?

Jumanne, 12 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wengi Wameitwa, Lakini Wachache Wanachaguliwa”

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Wengi Wameitwa, Lakini Wachache Wanachaguliwa”

Mwenyezi Mungu anasema, “Nawaita katika nyumba Yangu wale Niliowajaalia kulisikiliza neno Langu, kisha Nawaweka wote wanaotii na kulitarajia neno Langu mbele ya kiti Changu cha enzi. Wale wanaolisaliti neno Langu, wale wasiotii na kujisalimisha Kwangu, na wale wanaonipinga kwa wazi, watatupwa kando wakingoja adhabu ya mwisho. Wanadamu wote wanaishi katika upotovu na chini ya mkono wa yule mwovu, kwa hivyo sio wengi wanaonifuata wako na hamu ya ukweli kwa hakika.

Jumatatu, 11 Februari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Kuhusu Majina na Utambulisho" Sehemu ya Kwanza

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Kuhusu Majina na Utambulisho" Sehemu ya Kwanza

Mwenyezi Mungu anasema, "Yesu aliwakilisha Roho wa Mungu, na Alikuwa Roho wa Mungu Akifanya kazi moja kwa moja. Alifanya kazi ya enzi mpya, kazi ambayo hakuna aliyekuwa amefanya mbeleni. Yeye Alifungua njia mpya, Alimwakilisha Yehova, na Alimwakilisha Mungu Mwenyewe. Ilhali kwa Petro, Paulo na Daudi, bila kujali walichoitwa, waliwakilisha tu utambulisho wa kiumbe wa Mungu, ama walitumwa na Yesu na Yehova.

Jumapili, 10 Februari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu"

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu"

Mwenyezi Mungu anasema, "Bila kazi ya Yesu, mwanadamu hangeweza kushuka chini kutoka msalabani, lakini bila kupata mwili siku hii, wale wanaoshuka chini kutoka msalabani hawangewahi kusifiwa na Mungu ama kuingia katika enzi mpya. Bila kuja kwa huyu mwanadamu wa kawaida, basi hamngeweza kuwa na hii fursa ama kustahiki kuona uso wa ukweli wa Mungu, kwani nyinyi nyote ni wale ambao wangepaswa kuangamizwa kitambo sana.

Jumamosi, 9 Februari 2019

Maswali na Majibu ya Injili | Swali la 2

Swali la 2: Unashuhudia kwamba Mungu amekuwa mwili na kuwa Mwana wa Adamu ili kufanya kazi ya hukumu katika siku za mwisho, na bado wengi wa wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa wanakiri kwamba Bwana atarudi akija na mawingu, na wanategemeza hili hasa aya za Biblia: "Huyu Yesu … atakuja kwa namna hiyo hiyo ambayo mmemuona akienda mbinguni" (MDO 1:11). "Tazama, anakuja na mawingu; nalo kila jicho litamwona yeye" (UFU.1:7). Na zaidi ya hayo, wachungaji wa kidini na wazee wa kanisa pia hutufundisha kwamba Bwana Yesu yeyote asiyekuja na mawingu ni wa uongo na lazima aachwe. Kwa hiyo hatuna uhakika kama mtazamo huu unakubaliana na Biblia; ni sahihi kuchukua huu kama ukweli au la?

Ijumaa, 8 Februari 2019

4. Sura ya tatizo la mtu asiyejua umuhimu wa jina la Mungu na asiyelikubali jina jipya la Mungu ni ipi?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,  Yesu

IV. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Hatua Tatu za Kazi ya Mungu na Majina Yake

4. Sura ya tatizo la mtu asiyejua umuhimu wa jina la Mungu na asiyelikubali jina jipya la Mungu ni ipi?

Maneno Husika ya Mungu:
Mwenyezi Mungu alisema, Katika kila kipindi cha wakati, Mungu ataanza kazi mpya, na katika kila kipindi, patakuwepo na mwanzo mpya kwa mwanadamu. Laiti mwanadamu angeshikilia ukweli kwamba "Yehova ni Mungu" na "Yesu ni Kristo," ukweli ambao unazingatiwa kwa kipindi kimoja, basi mwanadamu hataweza kwenda sambamba na kazi ya Roho Mtakatifu, na daima hataweza kupokea kazi ya Roho Mtakatifu. Bila kujali jinsi Mungu anavyofanya, mwanadamu anafaa kufuata bila shaka lolote, na afuate kwa ukaribu.

Alhamisi, 7 Februari 2019

Ufafanuzi wa Mafumbo ya Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima | Sura ya 15

Sura ya 15

Mwenyezi Mungu alisema, Tofauti kubwa zaidi kati ya Mungu na mwanadamu ni kwamba kila mara maneno ya Mungu hugonga ndipo, na hakuna kilichofichwa. Kwa hiyo hali hii ya tabia ya Mungu inaweza kuonekana katika maneno ya kwanza ya leo. Kipengele kimoja ni kuwa yanaonyesha tabia halisi ya mwanadamu, na kipengele kingine ni kuwa yanafichua wazi tabia ya Mungu. Hizi ni asili kadhaa za jinsi maneno ya Mungu yanaweza kutimiza matokeo. Hata hivyo, watu hawalielewi hili, kila mara wao huja kujijua tu katika maneno ya Mungu lakini "hawajamchangua" Mungu.

Jumatano, 6 Februari 2019

Swahili Christian Music Video | "Ni Watu Waaminifu Pekee Walio na Mfano wa Binadamu" | God Led Me Onto the Right Path of Life

I
Kwa ajili ya faida niliacha viwango vyote vya mwenendo,
na bila haya nikatumia udanganyifu kutafuta riziki yangu.
Sikujali chochote kuhusu dhamiri au maadili, chochote kuhusu uadilifu au heshima.
Niliishi tu kuridhisha tamaa na uroho wangu vilivyozidi kukua.
Kwa moyo usio na amani, nilitembea katika matope ya dhambi,
bila njia yoyote ya kuepuka giza hii isiyo na mipaka.

Jumanne, 5 Februari 2019

3. Jina la Mungu linaweza kubadilika, lakini asili Yake haitabadilika kamwe.

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

IV. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Hatua Tatu za Kazi ya Mungu na Majina Yake

3. Jina la Mungu linaweza kubadilika, lakini asili Yake haitabadilika kamwe.

Maneno Husika ya Mungu:
Kuna wale ambao wanasema kuwa Mungu habadiliki. Hiyo ni sahihi, lakini inaashiria mabadiliko ya tabia ya Mungu na pia kiini chake. Mabadiliko ya jina lake na kazi hayathibitishi ya kuwa kiini chake kimebadilika; kwa maneno mengine, Mungu siku zote Atakuwa Mungu, na hii kamwe haitabadilika. Iwapo utasema kuwa kazi ya Mungu daima inabaki vile vile, basi Angekuwa na uwezo wa kumaliza mpango wake wa usimamizi wa miaka elfu sita?

Jumatatu, 4 Februari 2019

Fasiri ya Mafumbo ya Maneno ya Mungu | Sura ya 14

Fasiri ya Mafumbo ya Maneno ya Mungu | Sura ya 14

Mwenyezi Mungu alisema, Mwanadamu hajawahi kamwe kujifunza chochote kutoka kwa neno la Mungu. Badala yake, mwanadamu huthamini tu umbo la nje la neno la Mungu, lakini kutojua maana yake halisi. Kwa hivyo, ingawa wengi wa watu wanapenda neno la Mungu, Mungu asema kwamba hawalithamini kwa kweli. Hili ni kwa sababu katika maoni ya Mungu, hata ingawa neno Lake ni kitu cha thamani, watu hawajaonja utamu wake halisi.

Jumapili, 3 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Saba"

Maneno ya Roho Mtakatifu | "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima Tamko la Saba"

Mwenyezi Mungu anasema, "Nyie watu Wangu, myasikiapo maneno Yangu, je mnaielewa nia Yangu? Mnaiona roho Yangu? Mlipoipitia njia ya huduma hapo awali mlikumbana na panda-shuka, maendeleo mazuri na vikwazo, na zilikuwepo nyakati mlipokuwa katika hatari ya kuanguka na hata kunisaliti Mimi; lakini mlifahamu kuwa Nilikuwa katika harakati za kuwakomboa kila wakati? Kwamba kila wakati Nilikuwa napaza sauti Yangu kuwaita na kuwakomboa?

Jumamosi, 2 Februari 2019

1. Mungu aliwakomboa wanadamu katika Enzi ya Neema, hivyo kwa nini bado anahitaji kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu

III. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Kazi ya Mungu ya Hukumu katika Siku za Mwisho

1. Mungu aliwakomboa wanadamu katika Enzi ya Neema, hivyo kwa nini bado anahitaji kufanya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho?

Aya za Biblia za Kurejelea:
"Kwa hivyo mtakuwa watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu" (LAW. 11:45).
"Na utakatifu, bila huu hakuna mwanadamu atakayemwona Bwana" (EBR. 12:14).
"Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa mimi, na hayakubali maneno yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho" (YN. 12:47-48).
Maneno Husika ya Mungu:
Mwenyezi Mungu alisema, Wakati huo kazi ya Yesu ilikuwa ni ukombozi wa wanadamu wote. Dhambi za wote ambao walimwamini zilisamehewa; ilimradi wewe ulimwamini, Angeweza kukukomboa wewe; kama wewe ulimwamini Yeye, wewe hukuwa tena mwenye dhambi, wewe ulikuwa umeondolewa dhambi zako.

Ijumaa, 1 Februari 2019

9. Ni jinsi gani Mungu anayepata mwili ili kufanya kazi ya hukumu huimaliza imani ya wanadamu katika Mungu asiye yakini na enzi ya giza ya utawala wa Shetani?

I. Ni Lazima Mtu Ashuhudie Kipengele cha Ukweli Kuhusu Kupata Mwili kwa Mungu

9. Ni jinsi gani Mungu anayepata mwili ili kufanya kazi ya hukumu huimaliza imani ya wanadamu katika Mungu asiye yakini na enzi ya giza ya utawala wa Shetani?

Aya za Biblia za Kurejelea:
"Na itatimia katika siku za mwisho, kwamba mlima wa nyumba ya Yehova utawekwa imara juu ya milima, na utainuliwa juu zaidi ya vilima; na mataifa yote yatamiminika kwenda kwake. Na watu wengi wataenda na kusema, Njoo, na hebu twende juu ya mlima wa Yehova, kwa nyumba ya Mungu wa Yakobo; na atatufunza kuhusu njia zake, nasi tutatembea kwa njia zake: kwani sheria itatoka Zayuni, na neno la Mungu litatoka Yerusalemu. Naye atahukumu miongoni mwa mataifa, na atawakemea watu wengi: nao wata, nao watafua panga zao ili ziwe majembe, na mikuki yao ili iwe mundu: hakuna taifa litakaloinua upanga dhidi ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena. Enyi wa nyumba ya Yakobo, njooni, tutembee katika nuru ya Yehova" (ISA 2:2-5).